Qurani


KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU

سَأَلَ سَائِلٌ بِعَذَابٍ وَاقِعٍ
1.
Muulizaji aliuliza juu ya adhabu itakayo tokea,
لِّلْكَافِرِينَ لَيْسَ لَهُ دَافِعٌ
2.
Kwa makafiri - ambayo hapana awezaye kuizuia -
مِّنَ اللَّهِ ذِي الْمَعَارِجِ
3.
Kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mwenye mbingu za daraja.
تَعْرُجُ الْمَلَائِكَةُ وَالرُّوحُ إِلَيْهِ فِي يَوْمٍ كَانَ مِقْدَارُهُ خَمْسِينَ أَلْفَ سَنَةٍ
4.
Malaika na Roho hupanda kwendea kwake katika siku ambayo kadiri yake ni miaka khamsini elfu!
فَاصْبِرْ صَبْرًا جَمِيلًا
5.
Basi subiri kwa subira njema.
إِنَّهُمْ يَرَوْنَهُ بَعِيدًا
6.
Hakika wao wanaiona iko mbali,
وَنَرَاهُ قَرِيبًا
7.
Na Sisi tunaiona iko karibu.
يَوْمَ تَكُونُ السَّمَاءُ كَالْمُهْلِ
8.
Siku ambayo mbingu zitakapo kuwa kama maadeni iliyo yayushwa.
وَتَكُونُ الْجِبَالُ كَالْعِهْنِ
9.
Na milima itakuwa kama sufi.
وَلَا يَسْأَلُ حَمِيمٌ حَمِيمًا
10.
Wala jamaa hatamuuliza jamaa yake.
يُبَصَّرُونَهُمْ ۚ يَوَدُّ الْمُجْرِمُ لَوْ يَفْتَدِي مِنْ عَذَابِ يَوْمِئِذٍ بِبَنِيهِ
11.
Ijapo kuwa wataonyeshwa waonane. Atatamani mkosefu lau ajikomboe na adhabu ya siku hiyo kwa kuwatoa fidia wanawe,
وَصَاحِبَتِهِ وَأَخِيهِ
12.
Na mkewe, na nduguye,
وَفَصِيلَتِهِ الَّتِي تُؤْوِيهِ
13.
Na jamaa zake walio kuwa wakimkimu,
وَمَن فِي الْأَرْضِ جَمِيعًا ثُمَّ يُنجِيهِ
14.
Na wote waliomo duniani, kisha aokoke yeye.
كَلَّا ۖ إِنَّهَا لَظَىٰ
15.
La, hasha! Kwa hakika huo ni Moto mkali kabisa,
نَزَّاعَةً لِّلشَّوَىٰ
16.
Unao babua ngozi ya kichwa!
تَدْعُو مَنْ أَدْبَرَ وَتَوَلَّىٰ
17.
Utamwita kila aliye geuza mgongo na akageuka.
وَجَمَعَ فَأَوْعَىٰ
18.
Na akakusanya mali, kisha akayahifadhi.
إِنَّ الْإِنسَانَ خُلِقَ هَلُوعًا
19.
Hakika mtu ameumbwa na papara.
إِذَا مَسَّهُ الشَّرُّ جَزُوعًا
20.
Inapo mgusa shari hupapatika.
وَإِذَا مَسَّهُ الْخَيْرُ مَنُوعًا
21.
Na inapo mgusa kheri huizuilia.
إِلَّا الْمُصَلِّينَ
22.
Isipo kuwa wanao sali,
الَّذِينَ هُمْ عَلَىٰ صَلَاتِهِمْ دَائِمُونَ
23.
Ambao wanadumisha Sala zao,
وَالَّذِينَ فِي أَمْوَالِهِمْ حَقٌّ مَّعْلُومٌ
24.
Na ambao katika mali yao iko haki maalumu
لِّلسَّائِلِ وَالْمَحْرُومِ
25.
Kwa mwenye kuomba na anaye jizuilia kuomba;
وَالَّذِينَ يُصَدِّقُونَ بِيَوْمِ الدِّينِ
26.
Na ambao wanaisadiki Siku ya Malipo,
وَالَّذِينَ هُم مِّنْ عَذَابِ رَبِّهِم مُّشْفِقُونَ
27.
Na ambao wanaiogopa adhabu itokayo kwa Mola wao Mlezi.
إِنَّ عَذَابَ رَبِّهِمْ غَيْرُ مَأْمُونٍ
28.
Hakika adhabu ya Mola wao Mlezi si ya kuaminika nayo.
وَالَّذِينَ هُمْ لِفُرُوجِهِمْ حَافِظُونَ
29.
Na ambao wanahifadhi tupu zao.
إِلَّا عَلَىٰ أَزْوَاجِهِمْ أَوْ مَا مَلَكَتْ أَيْمَانُهُمْ فَإِنَّهُمْ غَيْرُ مَلُومِينَ
30.
Isipo kuwa kwa wake zao, au iliyo wamiliki mikono yao ya kuume, basi hao hawalaumiwi -
فَمَنِ ابْتَغَىٰ وَرَاءَ ذَٰلِكَ فَأُولَٰئِكَ هُمُ الْعَادُونَ
31.
Lakini wanao taka kinyume ya haya, basi hao ndio wanao ruka mipaka.
وَالَّذِينَ هُمْ لِأَمَانَاتِهِمْ وَعَهْدِهِمْ رَاعُونَ
32.
Na ambao wanazichunga amana zao na ahadi zao,
وَالَّذِينَ هُم بِشَهَادَاتِهِمْ قَائِمُونَ
33.
Na ambao wanasimama imara katika ushahidi wao,
وَالَّذِينَ هُمْ عَلَىٰ صَلَاتِهِمْ يُحَافِظُونَ
34.
Na ambao wanazihifadhi Sala zao.
أُولَٰئِكَ فِي جَنَّاتٍ مُّكْرَمُونَ
35.
Hao ndio watakao hishimiwa Peponi.
فَمَالِ الَّذِينَ كَفَرُوا قِبَلَكَ مُهْطِعِينَ
36.
Wana nini wale walio kufuru wanakutumbulia macho tu?
عَنِ الْيَمِينِ وَعَنِ الشِّمَالِ عِزِينَ
37.
Makundi kwa makundi upande wa kulia na upande wa kushoto!
أَيَطْمَعُ كُلُّ امْرِئٍ مِّنْهُمْ أَن يُدْخَلَ جَنَّةَ نَعِيمٍ
38.
Kwani kila mmoja wao anatumai kuingizwa katika Pepo ya neema?
كَلَّا ۖ إِنَّا خَلَقْنَاهُم مِّمَّا يَعْلَمُونَ
39.
La, hasha! Hakika Sisi tumewaumba kutokana na wanacho kijua.
فَلَا أُقْسِمُ بِرَبِّ الْمَشَارِقِ وَالْمَغَارِبِ إِنَّا لَقَادِرُونَ
40.
Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mashariki zote na magharibi zote kwamba Sisi tunaweza
عَلَىٰ أَن نُّبَدِّلَ خَيْرًا مِّنْهُمْ وَمَا نَحْنُ بِمَسْبُوقِينَ
41.
Kuwabadili kwa walio bora kuliko wao; na Sisi hatushindwi.
فَذَرْهُمْ يَخُوضُوا وَيَلْعَبُوا حَتَّىٰ يُلَاقُوا يَوْمَهُمُ الَّذِي يُوعَدُونَ
42.
Basi waache wapige porojo na wacheze, mpaka wakutane na siku yao wanayo ahidiwa,
يَوْمَ يَخْرُجُونَ مِنَ الْأَجْدَاثِ سِرَاعًا كَأَنَّهُمْ إِلَىٰ نُصُبٍ يُوفِضُونَ
43.
Siku watakapotoka makaburini kwa upesi kama kwamba wanakimbilia mfundo,
خَاشِعَةً أَبْصَارُهُمْ تَرْهَقُهُمْ ذِلَّةٌ ۚ ذَٰلِكَ الْيَوْمُ الَّذِي كَانُوا يُوعَدُونَ
44.
Macho yao yatainama, fedheha itawafunika. Hiyo ndiyo Siku waliyo kuwa wakiahidiwa.

Maelezo
Imeshuka: Makka
Ina aya: 44
Orodha ya Sura

1. AL-FATIHA
2. AL-BAQARAH
3. AL-'IMRAN
4. AL-NISA'
5. AL-MA'IDAH
6. AL-AN'AM
7. AL-A'RAF
8. AL-ANFAL
9. AL-TAWBAH
10. YUNUS
11. HUD
12. YUSUF
13. AL-RA'D
14. IBRAHIM
15. AL-HIJR
16. AL-NAHL
17. AL-ISRA
18. AL-KAHF
19. MARYAM
20. TAHA
21. AL-ANBIYA'
22. AL-HAJJ
23. AL-MU'MINUNE
24. AL-NUR
25. AL-FURQAN
26. AL-SHU'ARA
27. AL-NAML
28. AL-QASAS
29. AL-'ANKABUT
30. AL-RUM
31. LUQMAN
32. AL-SAJDAH
33. AL-AHZAB
34. SABA'
35. FATIR
36. YASIN
37. AS-SAFFAT
38. SAD
39. Al-ZUMAR
40. GHAFIR
41. FUSSILAT
42. AL-SHURA
43. AL-ZUKHRUF
44. AL-DUKHAN
45. AL-JATHIYAH
46. AL-AHQAF
47. MUHAMMAD
48. AL-FATH
49. AL-HUJURAT
50. QAF
51. AL-DARIYAT
52. AL-TUR
53. AL-NAJM
54. AL-QAMAR
55. AL-RAHMAN
56. AL-WAQI'AH
57. AL-HADID
58. AL-MUJADILAH
59. AL-HASHR
60. AL-MUMTAHANAH
61. AL-SAFF
62. AL-JUMU'AH
63. AL-MUNAFIQUN
64. AL-TAGHABUN
65. AT-TALAQ
66. AT-TAHRIM
67. AL-MULK
68. AL-QALAM
69. AL-HAQQAH
70. AL-MA'ARIJ
71. NUH
72. AL-JINN
73. AL-MUZZAMMIL
74. AL-MUDDATHTHIR
75. AL-QIYAMAH
76. AL-INSAN
77. AL-MURSALATE
78. AN-NABA'
79. AN-NAZI'AT
80. ABASA
81. AL-TAKWIR
82. AL-INFITAR
83. AL-MUTAFFIFIN
84. AL-INSHIQAQ
85. AL-BURUJ
86. AT-TARIQ
87. AL-A'LA
88. AL-GASHIYAH
89. AL-FAJR
90. AL-BALAD
91. AL-SHAMS
92. AL-LAYL
93. AL-DUHA
94. AL-SHARH
95. AT-TIN
96. AL-ALAQ
97. AL-QADR
98. AL-BAYYINAH
99. AL-ZALZALAH
100. AL-'ADIYAT
101. AL-QARI'AH
102. AT-TAKATHUR
103. AL-'ASR
104. AL-HUMAZAH
105. AL-FIL
106. QURAYSH
107. AL-MA'UN
108. AL-KAWTHAR
109. AL-KAFIRUN
110. AL-NASR
111. AL-MASAD
112. AL-IKHLAS
113. AL-FALAQ
114. AL-NAS