وَالذَّارِيَاتِ ذَرْوًا
|
1. |
Naapa kwa pepo zinazo tawanya,
|
|
فَالْحَامِلَاتِ وِقْرًا
|
2. |
Na zinazo beba mizigo,
|
|
فَالْجَارِيَاتِ يُسْرًا
|
3. |
Na zinazo kwenda kwa wepesi.
|
|
فَالْمُقَسِّمَاتِ أَمْرًا
|
4. |
Na zinazo gawanya kwa amri,
|
|
إِنَّمَا تُوعَدُونَ لَصَادِقٌ
|
5. |
Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka ni kweli,
|
|
وَإِنَّ الدِّينَ لَوَاقِعٌ
|
6. |
Na kwa hakika malipo bila ya shaka yatatokea.
|
|
وَالسَّمَاءِ ذَاتِ الْحُبُكِ
|
7. |
Naapa kwa mbingu zenye njia,
|
|
إِنَّكُمْ لَفِي قَوْلٍ مُّخْتَلِفٍ
|
8. |
Hakika nyinyi bila ya shaka mmo katika kauli inayo khitalifiana.
|
|
يُؤْفَكُ عَنْهُ مَنْ أُفِكَ
|
9. |
Anageuzwa kutokana na haki mwenye kugeuzwa.
|
|
قُتِلَ الْخَرَّاصُونَ
|
10. |
Wazushi wameangamizwa.
|
|
الَّذِينَ هُمْ فِي غَمْرَةٍ سَاهُونَ
|
11. |
Ambao wameghafilika katika ujinga.
|
|
يَسْأَلُونَ أَيَّانَ يَوْمُ الدِّينِ
|
12. |
Wanauliza: Ni lini hiyo siku ya malipo?
|
|
يَوْمَ هُمْ عَلَى النَّارِ يُفْتَنُونَ
|
13. |
Hiyo ni siku watakayo adhibiwa Motoni.
|
|
ذُوقُوا فِتْنَتَكُمْ هَٰذَا الَّذِي كُنتُم بِهِ تَسْتَعْجِلُونَ
|
14. |
Onjeni adhabu yenu! Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyahimiza.
|
|
إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي جَنَّاتٍ وَعُيُونٍ
|
15. |
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na chemchem.
|
|
آخِذِينَ مَا آتَاهُمْ رَبُّهُمْ ۚ إِنَّهُمْ كَانُوا قَبْلَ ذَٰلِكَ مُحْسِنِينَ
|
16. |
Wanapokea aliyo wapa Mola wao Mlezi. Kwa hakika hao walikuwa kabla ya haya wakifanya mema.
|
|
كَانُوا قَلِيلًا مِّنَ اللَّيْلِ مَا يَهْجَعُونَ
|
17. |
Walikuwa wakilala kidogo tu usiku.
|
|
وَبِالْأَسْحَارِ هُمْ يَسْتَغْفِرُونَ
|
18. |
Na kabla ya alfajiri wakiomba maghfira.
|
|
وَفِي أَمْوَالِهِمْ حَقٌّ لِّلسَّائِلِ وَالْمَحْرُومِ
|
19. |
Na katika mali yao ipo haki ya mwenye kuomba na asiye omba.
|
|
وَفِي الْأَرْضِ آيَاتٌ لِّلْمُوقِنِينَ
|
20. |
Na katika ardhi zipo Ishara kwa wenye yakini.
|
|
وَفِي أَنفُسِكُمْ ۚ أَفَلَا تُبْصِرُونَ
|
21. |
Na pia katika nafsi zenu - Je! Hamwoni?
|
|
وَفِي السَّمَاءِ رِزْقُكُمْ وَمَا تُوعَدُونَ
|
22. |
Na katika mbingu ziko riziki zenu na mliyo ahidiwa.
|
|
فَوَرَبِّ السَّمَاءِ وَالْأَرْضِ إِنَّهُ لَحَقٌّ مِّثْلَ مَا أَنَّكُمْ تَنطِقُونَ
|
23. |
Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, hakika haya ni kweli kama ilivyo kweli kuwa nyinyi mnasema.
|
|
هَلْ أَتَاكَ حَدِيثُ ضَيْفِ إِبْرَاهِيمَ الْمُكْرَمِينَ
|
24. |
Je! Imekufikia hadithi ya wageni wa Ibrahim wanao hishimiwa?
|
|
إِذْ دَخَلُوا عَلَيْهِ فَقَالُوا سَلَامًا ۖ قَالَ سَلَامٌ قَوْمٌ مُّنكَرُونَ
|
25. |
Walipo ingia kwake wakasema: Salama! Na yeye akasema: Salama! Nyinyi ni watu nisio kujueni.
|
|
فَرَاغَ إِلَىٰ أَهْلِهِ فَجَاءَ بِعِجْلٍ سَمِينٍ
|
26. |
Akenda kwa ahali yake na akaja na ndama aliye nona.
|
|
فَقَرَّبَهُ إِلَيْهِمْ قَالَ أَلَا تَأْكُلُونَ
|
27. |
Akawakaribisha, akasema: Mbona hamli?
|
|
فَأَوْجَسَ مِنْهُمْ خِيفَةً ۖ قَالُوا لَا تَخَفْ ۖ وَبَشَّرُوهُ بِغُلَامٍ عَلِيمٍ
|
28. |
Akahisi kuwaogopa katika nafsi yake. Wakasema: Usiwe na khofu, nao wakambashiria kupata kijana mwenye ilimu.
|
|
فَأَقْبَلَتِ امْرَأَتُهُ فِي صَرَّةٍ فَصَكَّتْ وَجْهَهَا وَقَالَتْ عَجُوزٌ عَقِيمٌ
|
29. |
Ndipo mkewe akawaelekea, na huku anasema na akijipiga usoni kwa mastaajabu, na kusema: Mimi ni kikongwe na tasa!
|
|
قَالُوا كَذَٰلِكِ قَالَ رَبُّكِ ۖ إِنَّهُ هُوَ الْحَكِيمُ الْعَلِيمُ
|
30. |
Wakasema: Ndivyo vivyo hivyo alivyo sema Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye hikima na Mwenye kujua.
|
|
قَالَ فَمَا خَطْبُكُمْ أَيُّهَا الْمُرْسَلُونَ
|
31. |
AKASEMA: Basi ujumbe wenu ni nini, enyi mlio tumwa?
|
|
قَالُوا إِنَّا أُرْسِلْنَا إِلَىٰ قَوْمٍ مُّجْرِمِينَ
|
32. |
Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwa watu wakosefu,
|
|
لِنُرْسِلَ عَلَيْهِمْ حِجَارَةً مِّن طِينٍ
|
33. |
Tuwatupie mawe ya udongo,
|
|
مُّسَوَّمَةً عِندَ رَبِّكَ لِلْمُسْرِفِينَ
|
34. |
Yaliyo tiwa alama kutoka kwa Mola wako Mlezi kwa ajili ya wanao pindukia mipaka.
|
|
فَأَخْرَجْنَا مَن كَانَ فِيهَا مِنَ الْمُؤْمِنِينَ
|
35. |
Kwa hivyo tutawatoa katika hao wale walio amini.
|
|
فَمَا وَجَدْنَا فِيهَا غَيْرَ بَيْتٍ مِّنَ الْمُسْلِمِينَ
|
36. |
Lakini hatukupata humo ila nyumba moja tu yenye Waislamu!
|
|
وَتَرَكْنَا فِيهَا آيَةً لِّلَّذِينَ يَخَافُونَ الْعَذَابَ الْأَلِيمَ
|
37. |
Na tukaacha humo Ishara kwa ajili ya wanao iogopa adhabu chungu.
|
|
وَفِي مُوسَىٰ إِذْ أَرْسَلْنَاهُ إِلَىٰ فِرْعَوْنَ بِسُلْطَانٍ مُّبِينٍ
|
38. |
Na katika khabari za Musa, tulipo mtuma kwa Firauni na hoja wazi.
|
|
فَتَوَلَّىٰ بِرُكْنِهِ وَقَالَ سَاحِرٌ أَوْ مَجْنُونٌ
|
39. |
Lakini alipuuza kwa sababu ya nguvu zake na akasema: Huyu ni mchawi au mwendawazimu!
|
|
فَأَخَذْنَاهُ وَجُنُودَهُ فَنَبَذْنَاهُمْ فِي الْيَمِّ وَهُوَ مُلِيمٌ
|
40. |
Basi tukamkamata yeye na majeshi yake na tukawatupa baharini, na yeye ndiye wa kulaumiwa.
|
|
وَفِي عَادٍ إِذْ أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمُ الرِّيحَ الْعَقِيمَ
|
41. |
Na katika khabari za A'di tulipo wapelekea upepo wa kukata uzazi.
|
|
مَا تَذَرُ مِن شَيْءٍ أَتَتْ عَلَيْهِ إِلَّا جَعَلَتْهُ كَالرَّمِيمِ
|
42. |
Haukuacha chochote ulicho kifikia ila ulikifanya kama kilio nyambuka.
|
|
وَفِي ثَمُودَ إِذْ قِيلَ لَهُمْ تَمَتَّعُوا حَتَّىٰ حِينٍ
|
43. |
Na katika khabari za Thamudi walipo ambiwa: Jifurahisheni kwa muda mdogo tu.
|
|
فَعَتَوْا عَنْ أَمْرِ رَبِّهِمْ فَأَخَذَتْهُمُ الصَّاعِقَةُ وَهُمْ يَنظُرُونَ
|
44. |
Wakaasi amri ya Mola wao Mlezi. Basi uliwanyakua moto wa radi nao wanaona.
|
|
فَمَا اسْتَطَاعُوا مِن قِيَامٍ وَمَا كَانُوا مُنتَصِرِينَ
|
45. |
Basi hawakuweza kusimama wala hawakuwa wenye kujitetea.
|
|
وَقَوْمَ نُوحٍ مِّن قَبْلُ ۖ إِنَّهُمْ كَانُوا قَوْمًا فَاسِقِينَ
|
46. |
Na kaumu ya Nuhu hapo mbele. Hakika hao walikuwa watu wapotovu.
|
|
وَالسَّمَاءَ بَنَيْنَاهَا بِأَيْدٍ وَإِنَّا لَمُوسِعُونَ
|
47. |
Na mbingu tumezifanya kwa nguvu na uwezo na hakika Sisi bila ya shaka ndio twenye uwezo wa kuzitanua.
|
|
وَالْأَرْضَ فَرَشْنَاهَا فَنِعْمَ الْمَاهِدُونَ
|
48. |
Na ardhi tumeitandaza; basi watandazaji wazuri namna gani Sisi!
|
|
وَمِن كُلِّ شَيْءٍ خَلَقْنَا زَوْجَيْنِ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ
|
49. |
Na katika kila kitu tumeumba kwa jozi ili mzingatie.
|
|
فَفِرُّوا إِلَى اللَّهِ ۖ إِنِّي لَكُم مِّنْهُ نَذِيرٌ مُّبِينٌ
|
50. |
Basi kimbilieni kwa Mwenyezi Mungu, hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake.
|
|
وَلَا تَجْعَلُوا مَعَ اللَّهِ إِلَٰهًا آخَرَ ۖ إِنِّي لَكُم مِّنْهُ نَذِيرٌ مُّبِينٌ
|
51. |
Wala msifanye kuwa kuna mungu mwengine pamoja na Mwenyezi Mungu. Hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake.
|
|
كَذَٰلِكَ مَا أَتَى الَّذِينَ مِن قَبْلِهِم مِّن رَّسُولٍ إِلَّا قَالُوا سَاحِرٌ أَوْ مَجْنُونٌ
|
52. |
Basi ndio hivyo hivyo, hakuwajia kabla yao Mtume ila walisema: Huyu ni mchawi au mwendawazimu.
|
|
أَتَوَاصَوْا بِهِ ۚ بَلْ هُمْ قَوْمٌ طَاغُونَ
|
53. |
Je! Wameambizana kwa haya? Bali hawa ni watu waasi.
|
|
فَتَوَلَّ عَنْهُمْ فَمَا أَنتَ بِمَلُومٍ
|
54. |
Basi waachilie mbali, nawe hulaumiwi.
|
|
وَذَكِّرْ فَإِنَّ الذِّكْرَىٰ تَنفَعُ الْمُؤْمِنِينَ
|
55. |
Na kumbusha, kwani ukumbusho huwafaa Waumini.
|
|
وَمَا خَلَقْتُ الْجِنَّ وَالْإِنسَ إِلَّا لِيَعْبُدُونِ
|
56. |
Nami sikuwaumba majini na watu ila waniabudu Mimi.
|
|
مَا أُرِيدُ مِنْهُم مِّن رِّزْقٍ وَمَا أُرِيدُ أَن يُطْعِمُونِ
|
57. |
Na sitaki kwao riziki, wala sitaki wanilishe.
|
|
إِنَّ اللَّهَ هُوَ الرَّزَّاقُ ذُو الْقُوَّةِ الْمَتِينُ
|
58. |
Hakika Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kuruzuku, Mwenye nguvu, Madhubuti.
|
|
فَإِنَّ لِلَّذِينَ ظَلَمُوا ذَنُوبًا مِّثْلَ ذَنُوبِ أَصْحَابِهِمْ فَلَا يَسْتَعْجِلُونِ
|
59. |
Hakika walio dhulumu wana fungu lao la adhabu kama fungu la wenzao. Basi wasinihimize.
|
|
فَوَيْلٌ لِّلَّذِينَ كَفَرُوا مِن يَوْمِهِمُ الَّذِي يُوعَدُونَ
|
60. |
Ole wao walio ikanusha siku yao waliyo ahidiwa.
|
|